• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

WALIMU WATAKIWA KUONGEZA KIWANGO CHA UFAURU

Imewekwa : August 12th, 2021

Maafisa Elimu ngazi ya wilaya na kata, Wakuu wa shule na walimu wakuu wamekutana na Kufanya kikao kazi cha pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila kwa lengo la kujiwekea mikakati katika kuongeza kiwango cha ufaulu kwenye  sekta ya elimu.

Akizungumza na walimu hao, Mkuu wa wilaya ya Muleba, Mhe. Toba Nguvila ameeleza kuwa kipaumbele chake ni elimu hivyo amewataka  walimu hao kuongeza kiwango cha ufaulu na kuwahaidi kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu ikiwemo uhaba wa miundombinu, changamoto za kiutumishi, maslahi yao na motisha.

" Naagiza kuanzia leo kuwepo na dirisha rasmi la kuwahudumia walimu wanapofika makao makuu ya wilaya na wapewe kipaumbele cha kusikilizwa ili wasitumie mda mwingi wilayani na kurudi kuwahudumia wanafunzi mashuleni" ameagiza Mhe. Toba Nguvila.

Katika kuwapa motisha walimu ili kuongeza kiwango cha ufaulu Mhe. Toba Nguvila ameeeleza kuwa hatuwezi kufanya vizuri bila kuwa na mikakati, amewahaidi kuongeza zawadi na kuanza kuwapa walimu watakaofaurisha vizuri katika masomo zawadi za viwanja ili kuzidi kuwatia moyo.

Sambamba na hilo Mhe. Toba Nguvila amehaidi kuanza matumizi ya TEHAMA shuleni kwa kutoa kompyuta kwa shule za Sekondari na Msingi na kwa kuanzia kwa muda wa mwezi mmoja wa utekelezaji wa majukumu yake wilayani Muleba tayari kuna shule nne mtaalamu amekuja na kubaini uhitaji wa vifaa hivyo na wakati wowote shule hizo zitapokea vifaa.

Wakitoa maoni yao walimu wameomba kuboreshewa miundombinu ikiwemo vyoo, madarasa na vyumba vya madarasa.Wialaya ione namna ya kuanzisha mabweni kwa ajili ya wanafunzi wanaotembea umbali mrefu kuja shuleni.

Elimu iendelee kutolewa kwa wazazi ili kuongeza mwamko wa elimu na kudhibiti utoro utoro mashuleni. Pia wameomba kuendelea kupewa fursa za kozi mbalimbali ili kuendana na hali halisi.

Aidha, Mhe. Toba Nguvila ameeleza katika kuunga mkono jitihada zake Naibu Waziri  wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Mathew amemuhaidi komyuta 10 kwa ajili ya shule zitakazoanzisha madarasa ya kompyuta.

Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa shule ya Sekondari Kishoju na kuhudhuriwa na walimu wakuu na wakuu wa shule wapatao 242 wa shule za msingi na sekondari, wa shule za Serikali na binafsi.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano, Halmashuri ya wilaya ya Muleba.


Matangazo ya kawaida

  • TANGAZO LA KARANTINI YA UGONJWA WA HOMA YA NGURUWE February 19, 2021
  • TANGAZO LA RUZUKU KUTOKA SERIKALI MKUU November 21, 2021
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA March 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • KAMATI YA MAJI YAAGIZWA KUWEKA ULINZI KWENYE VYANZO VYA MAJI

    August 19, 2021
  • SAMAKI WALIOVULIWA CHINI YA KIWANGO WAKAMATWA

    August 13, 2021
  • WALIMU WATAKIWA KUONGEZA KIWANGO CHA UFAURU

    August 12, 2021
  • MKURUGENZI MTENDAJI BW. ELIAS M. KAYANDABILA AKABIDHIWA OFISI RASMI

    August 11, 2021
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu: +255-756-350-183

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa